Censorship 2018-09-06T09:59:06+00:00
Man covering eyes of someone on their laptopMan covering computer user's eyes

Udhibiti ni kufichwa kwa maneno,picha ama mawazo kwa mfano kunyimwa haki ya kujieleza au kuongea na wenzako kwa jamii kwa sababu ujumbe huo unasemekana kuwa wa hatari ni mbaya.Hii hufanyika zaidi wakati ambapo watu wengine wanalazimisha ujumbe ,siasa au maadili yao kwa watu wengine.Udhibiti yaweza endelezwa na serikali ya nchi bila kusahau makundi ya binafsi na mashirika mengine.Kuna pia udhibiti wa kujitakia ambapo mtu anajinyima uhuru wa kujieleza kwa kuhofia kuteswa na serikali ama wenzake sanasana kwa kushikilia maoni tofauti kando na ambayo watu wanafahamu sana na ni kawaida kwao.

People searching for internet signal

Kuzimwa kwa mtandao katika mataifa ya Afrika

Kuathiriwa kwa mtandao kwa mfano kuzimwa kwa mitandao ya kijamii na saa zengine matumizi ya kutuma pesa kupitia rununu imeongezeka katika mataifa ya Afrika.Kuzimwa huku hufanyika zaidi nyakati za uchaguzi,fujo na hata majira ya mitahini ya kitaifa.Serikali na mahirika ya usalama zaweza surutisha mashirika za uwasilianaji kuzima mtandao kwa kusema kwamba ni jambo la usalama wa kitaifa na masharti.Katika taifa la Uganda kwa mfano mitandao ya kijamii na huduma za pesa kwa rununu zilizimwa mara mbili nyakati za uchaguzi mwaka wa 2016.

Kuzimwa kwa mtandao ni kutunyima haki yetu na uhuru wa kupata ujumbe,mawasiliano na ushirika kwa kutunyima nafasi ya kuzungumza na wenzetu na kutopata huduma muhimu.Serikali zafaa kuacha wananchi watumie mtandao ili kuongeza ushirika wao katika siasa.

Kunyamazishwa kwa wanahabari

Utafiti wa hivi majuzi waonyesha ongezeko wa uadui inayoelekezwa kwa vyombo vya habari ulimwenguni kote ambayo inaleta mashambulio mno kwa wanahabari na ata uhuru wa vyombo vya habari.Afrika mashariki haijaachwa nyuma.Wanahabari wamekuwa waathiriwa wa udhibiti wa binafsi ili kuzuia ghasia na kutishiwa.

Wanahabari ndio njia kuu ambayo wananchi wanaweza pata habari kupitia kwa vichapisho vya habari,radio na kupitia kwa runinga.Habari ya ukweli na sahihi ni ya muhimu sana kwa wananchi ili waweze kufanya maamuzi sawa hasaa kwa ushirika wao katika siasa na ata kwa utoaji wa huduma.Mara nyingi inakua vigumu kutathmini kwa uhakika kinachoendelea mjini Kampala ukiwa katika wilaya za mbali.Hivi wanahabari ndio macho na maskio yetu ndiposa wanafaa kulindwa ili waweze kufanya kazi yao vizuri bila hitilafu.

Journalist being beaten
Man receiving information requested

Kuafikia habari

Uganda ilikuwa kati ya nchi za kwanza kubuni sheria ya uhuru wa kupata habari.Sehemu ya kuafikia taarifa katika katiba 2005 na baadae uhuru wa kuafikia habari na kanuni 2011.Hii inaashiria kuwa kila mwananchi bila kuzingatia lolote ana haki na uhuru wa kuaafikia habari kutoka kwa serikali au mashirika mengine yanayowakilisha serikali.Hii ilibuniwa ili kuhakikisha utumizi kamili,uwazi na uwajibikaji wa serikali ili kuwapa wananchi nafasi ya kujihusisha katika maamuzi yanayowaathiri moja kwa moja kama vile utoaji wa huduma.

Cha kusikitisha mno ni kuwa kando na mipango hii yote,kuafikia habari muhimu kwa wanachi bado ni changamoto kubwa kwa sababu kadhaa kwa mfano kutosoma sheria,mifumo mirefu na mengineyo.Kuna hitaji kubwa kwa bunge na wananchi kuhakikisha kuwa uafikiaji wa habari unatimizwa kwa kuwahimiza watu na mashirika mbalimbali,utumiaji wa teknolojia kupunguza harakati ,kuboresha maarifa na ujuzi wa takwimu.

Ushawai jaribu kuafikia data ya jamii?

Man voting on a community project

Demokrasia sahihi ya kidigitali yaonekanaje?

Mtandao umewezesha kwa ukamilifu kizazi kipya kinachofahamu na watumizi wanaotaka mengi mno na zaidi inajenga kizazi kipya kinachojihusisha kwa kiwango kubwa na wenye ubaridi kwa serikali na siasa.

Kando na kutazama mtandao kama adui hasaa nyakati za uchaguzi,serikali ina nafasi nzuri ya kujihusisha zaidi na wananchi kwa mitandao ya jamii ili kuwawezesha kuchukua hatua za kimaarifa.Tafakari haya,kupata huduma zote za jamii kwa simu ya rununu au kupiga kura ukiwa nyumbani kwako bila hitilafu kwa tarakilishi.Huu ndio mstakabali wa serikali za kidijitali na demokrasia.

Kabla ya kuafikia haya yafaa tuhakikishe uafikiaji kwa wote ili kutoa tofauti zilizoko kwa sasa zisiwe kwa ulimwengu wa digitali.

Kushiriki katika siasa yafaa kuwahusisha watu wote kikamilifu?